ACHA UTOTO KWENYE FEDHA.

Kusimamia fedha zako binafsi ni mchakato unaoanza na kujua hali yako ya kifedha ya sasa; mchakato unaendelea na kuanzishwa na kuzingatia malengo yako, ili uweze kuendeleza mikakati ambayo itawawezesha kupata kutoka kwa hali yako ya sasa ili kufikia malengo yako. Upo usemi wa Kiswahili unaosema mtoto halali na hela. Umewahi kuuelewa vizuri? Kama bado, basi hiyo ndiyo inasababisha changamoto zako kifedha.

Mtoto halali na hela kwa sababu mtoto akipata hela hana siri, atamwambia kila mtu, atamringishia kila mtu, na wakati wote, atashika hela yake kwenye mkono wake. Sasa ukitaka kuipata fedha ya mtoto huyo, subiri alale, utaichukua kirahisi tu, na akiamka wala hatakuwa na kumbukumbu fedha hiyo imeenda wapi.

Hivi ndivyo watu wazima wengi wenye changamoto za fedha wanavyoishi. Wakipata fedha, iwe wamepokea mshahara, au wamepata faida, basi kila mtu atajua huyu ana fedha. Wataanza kutoa zawadi zisizo za msingi, wataanza kutoa ofa za vinywaji kwa watu, mtu atakutana na muuza nguo, hakuwa na mpango wa kununua nguo ila kwa kuwa amemuona na fedha anayo, basi ananunua.

Sasa jamii inapojua mtu ana fedha, na anazitoa kirahisi, kila mtu anatafuta mbinu ya kupata fedha hizo. Hapo sasa ndiyo utaona kila mtu anakuja na shida yake, shida ambayo kwa namna inaelezewa, utaona ni kubwa sana na wanahitaji msaada wako wa fedha, na kwa kuwa kila mtu anajua una fedha, basi huna budi bali kuchangia.

Hata matapeli wa fedha pia, wanafuata wale ambao wanaonekana wazi kwamba wana fedha, na wanakwenda na mitego ambayo ni vigumu kwa mtu kuing’amua.

Hivyo rafiki, hatua ya kwanza ya kutuliza fedha zako, acha utoto kwenye fedha, acha kuionesha dunia kwamba umepata fedha. Yaani kama kwa matendo yako tu mtu wa nje anaweza kujua una fedha au huna, wewe bado una tabia za kitoto kwenye fedha.

Jifunze nidhamu ya fedha jambo kubwa la kuzingatia ili uwe na nidhamu ya fedha binafsi au katika hatua ya kifamilia ni kuhakikisha unakua na bajeti na kuifuata. Kwamfano katika hatua ya undaaji bajeti kifamilia, si lazima kuwa na mshahara mkubwa kuwa bali ni kua tu nia ya kuendeleza ufanisi wa utekelezaji mambo ya kifamilia kwa kuzingatia vipaumbele kulingana na upatikanaji wa fedha (kipato). Kuna watu binafsi au familia nyingi zinafikiri kwamba bajeti sio kitu cha lazima sana kwao kwa sababu wao wana chanzo cha kawaida cha mapato na gharama zao za kila mwezi ni mfano wa familia yoyote ya wastani, kama kulipa kodi, bili za huduma, shule za watoto, au gharama za gari. Bila kujali uwepo wa bajeti katika uchumi wa familia, unasaidia kutafakari njia za kipato, inaweka wazi uwezo wa kipato, kuonyesha vipaumbele wa matumizi ya kipato, kusukuma utekelezaji huku na kutoa tahadhari. Hivyo unahitaji kuandaa bajeti yako binafsi au ya familia. Pia jijengee ukomavu kwenye fedha, ukomavu ambao ukiwa na fedha au ukiwa huna hakuna mabadiliko kwenye tabia. Hiyo itakuwezesha kutulia na fedha ambazo unazipata na kujiepusha na wanyonyaji wa fedha wanaokuzunguka.

Nakaribisha maswali na maoni.
Karibuni sana!
#Msanzya_2018
#Mfalme_wa_Michongo

Comments