Ufanisi unapatikana kwa kutokuwepo kwa makosa. Kadri
unavyopunguza utokeaji wa makosa unaongeza ufanisi. Kulingana na maandiko
matakatifu na taarifa mabalimbali za kitaalamu wanathibitisha kwamba binadamu
ni dhaifu katika namna moja au nyingine, hivyo kutokea kwa makosa katika
utendaji wake ni hali ya kawaida, ingawa kuna uwezekano mkubwa wa kuepuka makosa
ni finyu sana. Hivyo ukweli ni kwamba ili binadamu aweze kuepuka makosa katika
ufanyaji mambo yake anahitaji uwepo (utulivu wa akili na kuiweka akili yake
yote katika jambo au kitu tu anachokifanya wakati huo).
Kwa kuzingatia ukweli huu ni ni dhahili unapaswa kua na kitu
kimoja pekee cha kufanya, kwaajili ya kuboresha au kuimarisha ufanisi katika
ufanyaji mambo, hivyo ni vema zaidi au inapendeza zaidi na ina manufaa zaidi
katika ufanisi endapo ukichagua jambo moja tu, kitu kimoja tu au njia moja tu
ili uifanyie kazi (kulipa uwepo). Kulipa uwepo jambo moja inamaanisha kusahau
mengine yaliyopo na kuamini kua hayapo bali upo na jambo hilo moja tu.
Ukichagua jambo moja au kitu pekee cha kufanya unaongeza
ufanisi, ufanisi ukiongezeka utafanikiwa zaidi kuliko ukachagua mambo mawili au
zaidi mbayo ni mengi na itakupa kazi kuyapa uwepo yote kwapamoja, hivyo mwisho
wa siku mambo yote yatakushinda. Msemo wa Kiswahili unaosema “Mshika mbili,
moja humponyoka” unathibitisha jambo hili kwamba kama ukipendelea zaidi kufanya
mambo mawili au zaidi kwa wakati mmoja lazima itafika hatua utashika jambo moja
na mengine yatakushinda, yaani huwezi kushika mambo mawili kwa wakati mmoja “Mafahari
wawili, hawakai zizi moja” mambo mawili au zaidi huwezi kuyaweka katika akili
moja kwa wakati mmoja, lazima moja litasahaulika ili moja libaki.
Ili ufanikiwe katika hili, unahitaji kufanya maamuzi. Na uwezo
wa kufanya maamuzi ndicho kitu cha pekee kabisa unachopaswa kua nacho wakati wa
kufanya chaguzi (kuchagua) maana ndiyo msingi mkuu wakukupatia njia sahihi ya
kufuata, au jambo sahihi na bora zaidi la kusafanya maana si kila njia au jambo
nisahihi au linafaa kufanya pia kila njia au jambo linapishana ubora kati ya
njia au jambo moja na jingine. Pia uwezo
wa maamuzi ndio mtaji wa ufanyaji jambo, kitu au kufuata njia uliyoichagua. Hivyo
unapaswa kuchagua jambo lililosahihi na bora zaidi kuliko yote ndilo ufanye na
ufanye au njia bora zaidi ya kufuata na uifuate.
Pia unaweza kujifunza jinsi ya kutambua jambo au njia sahihi kwa kubofya kwenye maandishi ya bluu. JINSI YA KUTAMBUA JAMBO AU NJIA BORA NA SAHIHI
Aksante, nakaribisha ushauri, maswali na maoni.
Karibu!
#Msanzya_2018
#Mfalme_wa_Michongo
Innocent Leonard
Msanzya

Comments
Post a Comment